
Watu wengi huenda hawajui kama kukoroma ni ugonjwa. Kukoroma ni ugonjwa unaosababisha mtoto au mtu mzima kuacha kupumua akiwa usingizini hivyo anakuwa anashtuka na hivyo kushindwa kupata usingizi mzuri.
Wataalam wenyewe wanaita (Obstructive Sleep Apnea (OSA)). Hali hii ina madhara makubwa kwa mtoto. Haya ni baadhi ya madhara hayo
Sasa iwapo mwanao anakoroma mara kwa mara (angalau siku 3 kwa wiki) ama anakoroma kwa sauti na wakati mwingine unamuona kabisa anaacha kupumua, muone daktari wa pua na koo kama upo sehemu ambako wanapatikana. Sababu mojawapo kwa watoto wengi ni kuvimba kwa nyama za pua (adenoid) na mafindofindo(tonsil). Ukimuona daktari atakushauri tiba ipi inafaa.
Picha inaonyesha mtoto mwenye mafindofindo(tonsil)makubwa ambayo yanaweza kuziba kwa urahisi njia ya hewa na kusababisha mtoto kukoroma.













No comments:
Post a Comment