Sunday 17 May 2020

JPM-Nafikiria kufungua vyuo

Image may contain: 1 person, suit

“Wakati corona inaingia niliwaomba Watanzania tuombe kwa siku tatu, nashukuru sana Watanzania kwasababu wote tuliomba, tulifunga na Mungu amejibu na Mungu ametusikia, nashukuru sana Wachungaji, Masheikh, Maaskofu na Mungu ametusikia”-JPM



“Mungu ametusaidia na kwa taarifa za leo wagonjwa wamepungua sana Amana ilikuwa inalaza Watu 198, leo walikuwepo Watu 12 tu, Mlogonzila ilikuwa inalaza Watu 30 leo wamebaki 6, pale Kibaha Hospitali ilikuwa inalaza zaidi ya Watu 50 leo wamebaki Watu 22”
“Arusha moshono wamebaki 11, vituo vingine havina wagonjwa, Mwanza wana vituo kumi lakini wamebaki sita vituo vingine hakuna mgonjwa, Dodoma kuna vituo vinne kuna wagonjwa wawili walikuwa wagonjwa 42 wengine wote wamerudi nyumbani, Mungu amejibu maombi” 
#JPMChato

CHANZO: MillardAyo

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!