Wednesday 22 January 2020

Dr Boaz Mkumbo akifafanua kuhusu DAWA YA KISUKARI: Metformin

Kwa uelewa wangu kama Daktari, Sio kweli eti Unapokunywa Kidonge cha Metformin Kinakusaidia Utumie sukari ya kwenye wali, Ndizi,Ugali uliyokula. Hapana! Bali zinaenda kukusaidia kupambana na ongezeko la Sukari mwilini mwako. Swali ni Je Hii dawa inapambanaje?
.

Mfano: Ukila ndizi, Ukila wali, Ukila ugali, mwili Unachopokea kwenye damu ni “Sukari yaani Glukosi” Mwili wako hauna uwezo wa Kutambua “Hii ni glukosi ya ndizi,Glukosi ya wali,Glukosi ya Chapati au Mkate wa ngano” Hapana! Ukiupatia mwili wanga kwenye kinywa chako kinachofika kwenye damu ni GLUKOSI.

Vyanzo Vya Sukari mwilini huwa vipo viwili Kwanza ni Ini lako lina uwezo wa kutengeneza sukari kwa kubadilisha protini kuwa Sukari Gluconeogenesis na kubadilisha glycogen kuwa sukari yaani Glycogenolysis matendo hayo hata usipokula chakula chochote huzalisha takribani gram 200 za sukari kwa masaa 24.
.
Kiwango hicho cha sukari ambacho huzalishwa na mwili ndani bila kula sukari tunaita BASAL SUGAR na Hudhibitiwa kisipande sana na kiwango cha Insulin tunaita BASAL INSULIN.
.
Kwa mgonjwa wa Kisukari:
Mara tu unapokula chakula cha wanga na Ukanywa kidonge cha metformin. Kidonge hiki huenda kukusaidia KULIZUIA INI LISITENGENEZE SUKARI kwa sababu Likiachwa Litafanya SUKARI IPANDE ZAIDI. Pili dawa hii huwa inakuja KUVURUGA CHAKULA KISISAGWE VIZURI kwenye mfumo wa chakula Ili mwili UVUNE SUKARI KIDOGO.
.
Ume ona sasa? Dawa zinapigana kuzima Vyanzo vya SUKARI VYA NDANI wewe Unakula WANGA NYINGI ETI UKIJIPUMBAZA DAWA INAKUSAIDIA ILE WANGA ITUMIKE.
Hapana! Dawa Ina sehemu zake Mahusisi pakupunguzia sukari mwilini. Chakushangaza hata Ngumi ya Wali Ugali Pilau uliyo weka BADO ILE DAWA INAHANGAIKA KUHAKIKISHA SUKARI NYINGI HAIFIKI KWENYE MZUNGUKO WA DAMU.
.
Kama umenielewa Vizuri, Je Dawa hio Umeona Sehemu INAKUSAIDIA UTUMIE WANGA au SUKARI? Hapana!
Ili Mgonjwa Upate Nafuu Unatakiwa Usaidiane na Dawa kudhibiti sukari. Kama dawa inazuia vyanzo vya ndani vya SUKARI basi Italeta MAANA UKIBANA KUWEKA VYANZO VYA NJE VYA SUKARI.
Yaani “Kile dawa inacho enda Kukisumbukia Kukishusha basi Punguza KUWEKA"
TUMIA DAWA ONGEZA UMAKINI NA CHAKULA


Kwa hisani ya
Dr. Boaz Mkumbo MD

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!