Monday 2 October 2017

Mshambuliaji Stephen Paddock aua watu 58 Las Vegas, Marekani

People fleeing from scene of country music festival
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionZaidi ya watu 50 wauawa kwa wapigwa risasi Las Vegas Marekani
Zaidi ya watu 58 wameuawa na takriban 515 kujeruhiwa kwenye ufyatuaji wa risasi wakati wa tamasha la muziki huko Las Vegas, Marekani.


Mtu mwenye bunduki mwenye umri wa maika 64 Stephen Paddock alifyatua risasi kutoka ghoroga ya 32 kwenye hoteli ya Mandalay Bay, kwenda kwa tamasha lililokuwa likiendelea nje.
Eneo la mauaji
Image captionEneo la mauaji
Polisi wanasema mshukiwa ambaye alitajwa kuwa makaazi wa mji huo na ambaye hakutajwa jina ameuawa.
Mamia ya watu walikimbia eneo hilo na milio ya risasi ikasikika kwa muda kwenye video zilizochapishwa katika mitandao ya kijamii.
Ufyatuaji huo ulitokea mwendo wa saa 05:30 GMT na walioshuhudia walisema kuwa mamia ya risasi zilifyatuliwa.
Usafiri wa ndege ulisitishwa kutoka uwanja wa ndege wa McCarran mjini Las Vegas

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!