Monday 28 March 2016

AJALI: Basi la Super Shem (Lupondije) laanguka Ruaha, Iringa na kuua wanne usiku huu



Kuna basi la Super Shem limeanguka mlima wa Ruaha Iringa. Inasemekana hali za abiria ni mbaya.



Basi hilo lilikuwa likitokea Mwanza kwenda mbeya.

Waliofariki ni wanne. Wanaume wawili na wanawake wawili.

Majeruhi ni 38, wako hospitali ya mkoa, Iringa. Basi hili lilikuwa la kuishia Iringa ila kuna abiria waliokuwa wakipelekwa Ipogolo kufaulishwa kwenye gari la Mbeya na wakati linashusha ule mlima ndio likafeli breki na kugonga kingo za barabara na kuanguka.

Majeruhi wengi wamevunjika viungo.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!