Thursday 25 February 2016

ECZEMA KWA WATOTO:UKAVU WA NGOZI,KUWASHWA NGOZI ,DALILI YAKE NA MATIBABU

image

Eczema(atopic dermatitis) ni ugonjwa wa ngozi ,unaofanya ngozi kuwasha sana kuwa kavu na kupata vijipele vidogo vidogo vyenye rangi nyekundu,huu ugonjwa ushambulia watoto na  wakubwa sehemu za viungo vya mwili (joints) mkononi


Shingoni na miguuni na inaweza tokezea sehemu ya usoni ,juu ya jicho ,makwapani,mgongoni ,tumboni ,mbele ya kichwa (forehead),mapajani,mdomoni na mashavuni. Watoto walio chini ya miaka 5 huwa adhiri  kwa asilimia 15% unaweza chukua mda kupona kulingana na ngozi na kiasi cha mtoto alivyoadhirika.



Chanzo cha ugonjwa wa eczema

Eczema inasababishwa na mwili kushindwa kutengeneza au kuzalisha ceramider ,ceramider ni fatty cell inayotumika kwenye uzalishwaji wa ngozi,ceramider inaposhindwa kuzalishwa ngozi ya mtoto inapoteza kiwango cha maji na kuifanya kuwa kavu na ndipo inapomso sababishia kuanza kujikuna ,ngozi kuwa kavu na kubadilika rangi kuwa nyekundu.

  • Eczema ni ugonjwa wa kuridhi -toka kwa mama / baba aliekuwa na ugonjwa  ni rahisi mtoto akaridhi.

  • Mzingo(Allergy au asthma)na pumu huleta eczema



Nini kinachochea kutopona eczema haraka kwa mtoto

Mtoto mwenye tatizo la eczema anatakiwa aepushwe

  • Ngozi kuwa kavu (dry skin)-epuka ngozi ya  mtoto kuwa kavu itasababisha kuwa na low humidity na kujikuna sana .

  • Joto kali-joto linapokuwa kali inamsababisha mtoto kujikuna zaidi ,usimveshe mtoto nguo nyingi kipindi cha joto itamfanya ajikune sana .

  • Food allergy-kuna baadhi ya vyakula vyenye kuleta allergy inatakiwa asipewe kama maziwa,mtindi,mayai,cheese ,nuts(karanga,korosho nk)mikate,pweza,kamba

  • Acid fruits-matunda yen acid asitumie ndimu ,machungwa,nyanya,strawbell

  • Acha kutumia vitu vya harufu kali kama sabuni ,perfumes ,majani,na mafuta

  • Kuogeshwa kwa mda mrefu-epuka kumwogesha kwa mda mrefu au kukaa ndani ya maji isizidi dakika 10 maji yana sababisha ngozi kuwa kavu zaidi,atumie maji vugu vugu wakati wa kumwogesha tumia sabuni ya (sensitive skin) isiyo na harufu na usitumie shampoo

  • Nguo za kumbana-usimveshe nguo za kumbana au zenye matrial ya synthetic fabric, wool, ,mveshe nguo za kupwaya ziwe material ya cotton inamfanya ajisikie vizuri bila miwasho.

  • Nguo mpya-nguo mpya inamfanya ajikune zaidi ,kabla ujamvesha fua kwanza.

  • Sabuni ya kufulia nguo -nayo inaweza msabishia kuwashwa zaidi ,fatilia kila ufuapo kama ukimvesha izo nguo na kuwashwa sana ujue iyo sabuni haimfai

  • Kucha kuwa ndefu-zitamkwarua na kujikuna sana kuharibu ngozi zaidi ,hakikisha kucha zake ni fupi kila mara.





Tiba

Eczema kutibika  kwa haraka ni ngumu ,kuna dawa za kupaka na ikapunguza muwasho, fatilia masharti hayo nilioandika hapo juu na kula matunda na mboga mboga kwa wingi

image

yanayoweza tibu au punguza eczema kwa kiasi kama  parachichi ,ndizi mbivu, papai,apple,juice ya carrots ,tango,aloe vera,spinanch ,viazi vitamu,viazi ulaya,smoothie ya tango,parsley,broccoli na tangawizi kidogo saga pamoja wapewe kwa watoto walio juu ya miezi 6 ,samaki wa maji baridi kama salmon wanafaa zaidi wana omega 3 ya kutosha.Mwepushe mtoto kula fast food zinachochea ugonjwa kuongezeka.

 image

Eczema inaweza itachukua  mda  mtoto kupona akuavyo ndivyo ugonjwa unapotea.Utakapo ona mtoto wako ana dalili ya eczema mpeleke kwa pediatriacian  au dermatolost atampima na atamwandikia antiobioc na cream za kutumia kupunguza kujikuna.


Mpake kimoja wapo kati ya hivi  mafuta ya nazi ,lotion, ointments au creams mara kwa mara  unapo ngozi yake ipo kavu,akitoka kuoga usichelewe kupaka mafuta

  • Mveshe mtoto nguo ya mkono mrefu usiku akitaka kulala ili asijikune

  • Mwepushe kumpa vyakula vya kukaangwa

  • Asile vyakula vyenye spices(viungo) ukipika chakula cha familia tenga mboga yake kabla ujaweka spices.

Home remedies

Unaweza kutengeneza dawa ya eczema kwa kutumia vitu asilia

Mahitaji

vijiko 3 vya extra virgin olive oil

kijiko kimoja cha baking soda

vijiko 2 vya oats iliosagwa


Jinsi ya kuandaa

Weka maji kwenye beseni au ndoo changanya na huo mchanganyiko  koroga  wacha huo mchanganyiko kwa dakika 15-20 ndio aogee

inamsaidia ngozi kuwa ng’aavu na laini itaondoa ile hali ya kujikuna.




Dawa nzuri za eczema – Aveeno baby,Eucerin,proecza,,Aquaphor,cetaphir,Dermatex,Diprobase,Ezerra na nyinginezo onana na daktari wa watoto kabla ujanunua dawa na atakapo tumia uwe mvulimivu sio kitu cha kupona haraka ila mabadiliko utayaona kwa mda mfupi tu.


SHUKRANI KWA AFYA YA MAMA NA MTOTO

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!