Friday 15 January 2016

Sierra Leone yaripoti kisa cha ebola

Image copyrightAFP
Image captionSierra Leone yaripoti kisa chengine cha ebola
Siku moja tu baada ya shirika la afya duniani WHO kutangaza kumalizika kwa Ebola huko Afrika magharibi ,maafisa wa Sierra Leone wamesema wanachunguza kifo kimoja cha mgonjwa ambacho sasa kimebainika kimetokana na Ebola.


Ebola imesababisha vifo vya zaidi ya watu elfu 11 katika mataifa ya Guinea, Liberia na Sierra Leone tangu kutokea kwa mlipuko wa ugonjwa huo miaka miwili iliyopita.
Taifa hilo lilitangazwa kuangamiza Ebola mnamo mwezi Novemba, na eneo hilo kwa jumla lilitangazwa lisilo na ugonjwa huo baada ya Liberia kutangazwa kuumaliza ugonjwa huo siku ya Alhamisi.
Vipimo vilivyofanyiwa mtu huyo aliyefariki kutokana na ugonjwa huo kaskazini mwa Sierra Leone vilithibitisha hilo,msemaji wa kituo kimoja cha kupima ugonjwa huyo aliiambia BBC.
Image copyrightAFP
Image captionMtu aliyefariki kutokana na ugonjwa wa ebola
Shirika la afya duniani WHO limeonya ,hatahivyo kwamba linatarajia hisia kali kutolewa.
Kifo hicho kilitokea mapema wiki hii.Shirika la habari la Reuters limeripoti kwamba mwathiriwa ni mwanafunzi wa miaka 22.
Shirika hilo pia limesema kwamba lina habari kutoka kwa shirika moja la hisani kwamba mgonjwa huyo alitibiwa kama mgonjwa wa kuingia na kutoka.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!