skip to main |
skip to sidebar
SALAD YA KABICHI
Mahitaji
- Kabichi 1
- Pilipili hoho 1
- Karoti 2
- Vitunguu maji 2
- Kitunguu saumu 1
- Limao au ndimu
- Tangawizi 1
- Mafuta vijiko 3 (olive oil)
- Chumvi
Maelekezo
- Katakata kabichi, pilipili hoho, karoti, kitunguu maji. Twanga kitunguu saumu na tangawizi.
- Osha kabichi, iweke ichuje maji alafu inyunyizie chumvi.
- Changanya pilipili hoho, karoti na kitunguu maji kwenye kabichi.
- Kamulia limao au ndimu.
- Bandika sufuria, weka mafuta yakipata moto weka kitunguu saumu na tangawizi.
- Koroga mpaka viive, weka kabichi koroga kwa muda wa dakika 5. Epua halipendezi likiiva sana, hapo ni muda wa kujiramba.
No comments:
Post a Comment