Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Kazimili (49) Mkazi wa Kitongoji cha Misenga Tarafa ya Mwese ameuwawa kikatili kwa kukatwa katwa na shoka na mapanga katika sehemu mbalimbali za mwili wake wakati akiwa amelala chumbani kwake na mke wake.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwaambia waandishi wa Habari jana kuwa tukio la mauwaji hayo ya kikatili lilitokea hapo juzi majira ya saa saba usiku nyumbani kwa marehemu huyo .
Alisema siku hiyo ya tukio marehemu alikuwa amelala kwenye nyumba yake ndani ya chumba chake akiwa na mke wake waliyekuwa wakiishi nae pamoja na watoto wake .
Kidavashari alieleza wakati marehemu akiwa amelala ndani watu wasiofahamika walifika nyumbani kwake na kuvunja mlango wa mbele wa nyumba yake hiyo huku wakiwa na silaha aina ya shoka na mapanga.
Baada ya kuwa wamevunja mlango wa mbele watu hao waliingia ndani hadi mahali alipokuwa amelala marehemu na mkewe na kisha walimtowa sebuleni marehemu huku wakiwa wamemlazimisha mkewe asitoke nje wala asipige kelele.
Kidavashari alieleza baada ya kuwa wamemtowa sebuleni walianza kumshambulia kwa kumkatakata kwa silaha za panga na shoka katika seheme mbalimbali za mwili wake za kichwani shingoni na kwenye mikono yake huku marehemu huyo akiwa anapiga mayowe ya kuomba msaada kwa majirani zake.
Alisema pamoja na marehemu kupiga mayowe wauwaji hao hawaku jali na waliendelea kumkatakata marehemu hadi walipoona amefariki dunia ndipo walipotokomea kusiko julikana.
Majirani walifika kwenye eneo hilo na walikuta mwili wa marehemu ukiwa umegalagala chini huku ukiwa umekatwa katwa katika sehemu mbalimbali za mwili wake.
Kamanda Kidavashari alisema mpaka chanzo cha kifo hicho cha mauwaji ya kikatili hakijafahamika na jeshi la pollsi wa kushirikiana na wananchi wa Kitongoji hicho wanaendelea na msako wa kuwatafuta watu waliohusika na mauwaji hayo.
No comments:
Post a Comment