Monday 1 June 2015

KIM KARDASHIAN AFICHUA NI MJAMZITO, KUZAA MTOTO WA PILI

Mmwanamitindo wa Marekani, Kim Kardashian akiwa na mumewe mwanamuziki, Kanye West.


Kim Kardashian akifanyiwa vipimo hospitalini jana, ambapo alionekana kuwa mjamzito.  Aliyesimama kushoto ni mama yake, Kris Jenner.
Mojawapo ya vipimo alivyofanyiwa Kim katika kuhakikisha ni mjamzito
MWANAMITINDO wa Marekani, Kim Kardashian, hivi sasa ni mjamzito akitegemea kumpatia mumewe, mwanamuziki, Kanye West, mtoto wa pili.
Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 34, na ambaye mtoto wake wa kike aitwaye North atatimiza miaka miwili tarehe 15 mwezi huu, aliyasema hayo kwenye kipindi cha televisheni Jumapili cha ‘Keeping Up With The Kardashians’.
Nyota huyo alimwambia dada yake Khole: “Nimepima damu hivi karibuni na nina ujauzito!” Wakati ndugu zake wakishangaa, mama yake, Kris Jenner, alisema anamsubiri mjukuu wake kwa hamu kubwa.
Kim alizaa mtoto wake wa kwanza Juni 15, 2013, na akafunga ndoa na Kanye Mei 24, 2014.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!