
MSHAMBULIAJI wa Yanga, Amissi Tambwe, ameweka wazi kwamba mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Ruvu Shooting ambayo walimaliza kwa suluhu juzi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar, haikuwa ya soka na yeye alinusurika kuuawa.
Tambwe amesema ni mechi itakayobaki kwenye kichwa chake kwa mambo mawili, kwanza ni beki George Michael ‘beki mkatili’ ambaye alimpiga kiwiko kwenye jicho na mdomoni.
Osei wa Ruvu akizikunja na Tambwe.
Osei (kulia) akisukumana na Tambwe.
Pili ni maneno makali yaliyoupasua moyo wake baada ya kuitwa mkimbizi na kukumbushiwa vita ya wenyewe kwa wenyewe inayoendelea nchini Burundi.
Katika mahojiano na Championi Jumatatu, Tambwe amesema Michael alimkaba kwa nguvu zaidi ya mara moja na kumfanya ashindwe kupumua.
“Haukuwa mpira, hauwezi kuamini kama kweli wale walikuja uwanjani kucheza soka. Walinipiga kiwiko, wakanipiga ngumi na mwisho Michael alinikaba shingoni zaidi ya mara moja na kunifanya nishindwe kupumua.
“Haukuwa mpira, hauwezi kuamini kama kweli wale walikuja uwanjani kucheza soka. Walinipiga kiwiko, wakanipiga ngumi na mwisho Michael alinikaba shingoni zaidi ya mara moja na kunifanya nishindwe kupumua.
“Hii ni hatari, kuna mtu anaweza kuanguka akapoteza maisha siku moja. Wale wanajeshi hawaingii uwanjani kucheza soka, wanakwenda kucheza na mwili wa wachezaji wenzao.
“Ila nilishangazwa na mwamuzi kutoa kadi kwetu huku akionekana kuwahofia wanajeshi. Ukimwambia mwamuzi anachekacheka tu, sijui alikuwa anamaanisha nini.
“Ila nilishangazwa na mwamuzi kutoa kadi kwetu huku akionekana kuwahofia wanajeshi. Ukimwambia mwamuzi anachekacheka tu, sijui alikuwa anamaanisha nini.
No comments:
Post a Comment