
Wanafunzi 150 kati ya 1,000 waliojiunga na masomo
katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (Duce)
mwaka jana wamebainika kuwa na ujauzito waliopewa
na wenzao chuoni hapo.
kati ya Juni na Novemba mwaka jana umebaini kuwa
wanafunzi wanaopata ujauzito ni wale wa mwaka wa kwanza.
Hayo yamebainishwa jana na Mratibu wa Masuala ya Jinsia
Hayo yamebainishwa jana na Mratibu wa Masuala ya Jinsia
wa chuo hicho, Dk Dativa Shilla katika warsha ya uchaguzi
na uhusiano wa kijinsia iliyofanyika chuoni hapo.
Alisema hali hiyo inatokana na kuwapo kwa vitendo vya ukatili, manyanyaso na ubabe unaofanywa na wanachuo wa kiume dhidi ya wale
Alisema hali hiyo inatokana na kuwapo kwa vitendo vya ukatili, manyanyaso na ubabe unaofanywa na wanachuo wa kiume dhidi ya wale
wa kike na hivyo kuwalazimisha kufanya mapenzi bila
hiyari yao.
“Kupitia utafiti huu tumeona hakuna usawa wa kijinsia
“Kupitia utafiti huu tumeona hakuna usawa wa kijinsia
wa kupata elimu baina ya mwanamke na mwanamume
kwa sababu mwenye ujauzito hawezi kufanya vizuri
katika masomo yake ukilinganisha na mhusika wa kiume,”
ya Mwalimu Nyerere, Amon Katunzi alisema ni wakati sasa
kwa Serikali kutoa mikopo kwa wanafunzi wote kwa sababu
hatua hiyo itapunguza wanafunzi wa kike kujiingiza
katika uhusiano wa kimapenzi kwa sababu watakuwa
na fedha za kujikimu.
“Lengo la warsha hii ni kutoa elimu na ushauri kwa wanafunzi
“Lengo la warsha hii ni kutoa elimu na ushauri kwa wanafunzi
wa jinsi zote ili waweze kusoma vizuri na kuacha ushawishi
wa kujihusisha na uhusiano wa kimapenzi. Pia, tunawashauri
hata wale ambao wapo katika ndoa wavumilie na kuepuka
kupata ujauzito ili waweze kufanya vizuri katika masomo yao,” alisema Katunzi.
Mwanafunzi wa mwaka wa pili katika chuo hicho Gosbeth
Mwanafunzi wa mwaka wa pili katika chuo hicho Gosbeth
Kihanga ambaye alikiri kuwapo kwa vishawishi chuoni
hapo na kudai kuwa inachangiwa na ugumu wa maisha
hasa kwa wanafunzi wa kike.
Alisema kupitia kongamano hilo wamejifunza na kuelewa
Alisema kupitia kongamano hilo wamejifunza na kuelewa
mengi hususani katika suala la kupanga na kugawana
majukumu, kubadilisha mtazamo na kuacha kutumia ubabe
katika uhusiano wa mapenzi.
Chanzo: mwananchi.co.tz
Chanzo: mwananchi.co.tz
No comments:
Post a Comment