

Mmoja wa majeruhi katika tukio hilo la moto akisimulia.
AKizungumza Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Naibu Kamishna Mohammed Mpinga, alisema ajali hiyo haikuleta athari yoyote baada ya gari lile kupata ajali ila athari ilijitokeza baada ya watu kuvamia na kuanza kuiba mafuta na baadaye kujaribu kuiba betri ndipo cheche za moto zilipolipuka na kusababisha kuwaka kwa gari hilo.
Wakati huohuo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mecky Sadick, amewataka wananchi kutokuwa na tabia ya kuvamia ama kuiba vitu pindi ajali zitokeapo.
Sadick alisema hayo alipotembelea hospitali ya Muhimbili na Temeke walipolazwa majeruhi hao.
No comments:
Post a Comment