Wednesday, 16 July 2014

KAMPUNI YA BHAKRESA YATOA CHEKI YA DOLA ZA MAREKANI 93,000 KUISADIA TIMU YA RIADHA YA TAIFA.


images

NAIBU WAZIRI wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Mhe. Juma Nkamia amemuomba  mmiliki wa kiwanja cha michezo cha Azam Complex Bw. Said Salim Bakhresa  kutoa ruhusa kwa wachezaji wa Tanzania kufanya mazoezi katika  uwanja huo hasa wakati wa usiku ili ziweze kuwa katika nafasi nzuri na zipate uzoefu wa kucheza muda huo.

 
Hayo yamesemwa leo na Mhe. Nkamia katika kikao  cha kukabidhiwa cheki na  Bw. Bakhresa  yenye thamani ya Dola 93,000 ili kuisaidia timu ya Taifa ya riadha kufika Glasgow, Scotland pamoja na mahitaji mengine kama  jezi na vifaa.
 
 “Fedha hii  itasaidia timu yetu yenye wachezaji 39 ,makocha, pamoja na  walimu waliotoka China kuweza kurudi salama.” Alisema Nkamia.
 
Aidha, Mhe. Nkamia ametoa pongezi  kwa  Rais wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuweza kuzungumza na wachezaji hao na kuwakabidhi bendera ya Taifa huko waendako.
 
Bw. Bakhresa amesema kuwa anaisapoti timu ya Taifa kwenda Scotland kwa sababu michezo siyo mpira wa miguu tu na amefafanua kuwa mashindano ya michezo ni kitu muhimu katika nchi na kinaleta maendeleo.
 
“Tunachokipata kinatokana na jasho la watanzania na tunakirudisha kwa watanzania,Tanzania inajengwa na watanzania wenyewe siyo watu wa nje”. Alisema Bakhresa.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!