Saturday 21 June 2014

UINGEREZA NJE YA KOMBE LA DUNIA.


Uingereza imebanduliwa nje ya kombe la dunia Brazil.
Uingereza wameondolewa kutoka kombe la dunia la mwaka huu huko Brazil baada ya raundi ya kwanza, kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1958.


Uingereza ilibanduliwa baada ya Italia kupoteza mechi yao dhidi ya Costa Rica 1-0 huko Recife katika kundi D.

Uingereza ilihitaji Italia kushinda mechi yao ili wapate matumaini ya kuendelea lakini Costa Rica walipoishinda Italia, matumaini yao yakapotea pia.Uingereza ilikuwa imeshindwa na Uruguay na Italia katika mechi zilizotangulia.
Kikosi cha Uingereza kiliitazama mechi hiyo kutoka katika makazi yao, hotelini huko Rio.
Aliyekuwa mlinzi katika kikosi hicho, Rio Ferdinand anaamini kuwa kukosa uzoefu kulichangia pakubwa katika kuondolewa kwa timu hiyo mapema hivyo.

Ushindi wa Costa Rica umeiondoa Uingereza
Hata hivyo anadhani kuwa mchuano huo ni muhimu kwani utasaidia kukuza wachezaji wao wachanga.
“labda Uingereza ilikua bado changa katika hali tofauti .
Mfano, katika mchuano dhidi ya Uruguay, waliposawazisha 1-1, walikua na nafasi ya kupata angaa alama moja na hilo lingekua bora” alisema Ferdinand.
Mkufunzi Roy Hodgson, alichagua kikosi kilichokua na wachezaji wachanga na alitumai watanawiri kutoka kwa kundi lao gumu.
Kwa natharia, Costa Rica ndio iliyotarajiwa kulazwa mabao mengi ikilinganishwa na majina makubwa katika kandanda Hata hivyo, Costa Rica ndio wamekuwa wa kwanza kuingia katika raundi ya pili.

Uingereza imebanduliwa nje ya kombe la dunia Brazil.
Hata ingawa walishindwa katika mechi yao ya kwanza na timu ya Italy 2-1, mechi yao ya Alhamisi dhidi ya Uruguay ilionekana kuwapa matumaini.
Uruguay walikuwa wamepoteza mechi yao ya kwanza dhidi ya Costa Rica.
Hata hivyo, mabao mawili ya Luis Suarez yaliipatia Uruguay ushindi wa 2-1, tukio lililowaacha wachezaji wa Uingereza kutegemea matokeo ya michuano mingine,
Baada ya kushindwa Hodgson alisisitiza kuwa hataacha kuwa mkufunzi wa Uingereza, naye Greg Dyke, mkuu wa shirikisho la soka la Uingereza (FA), akimhakikishia Hogson kuwa kibarua chake hakijaota nyasi.

Uingereza watamaliza kampeni yao dhidi ya Costa Rica siku ya Jumanne

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!