Friday, 27 June 2014
SHIRIKA LA UTANGAZAJI TBC LAPATIWA MSAADA WA GARI LA KISASA LA KURUSHIAMATANGAZO
Msafara wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Li Yunchao ukiwasili katika Viwanja vya Ofisi za Shirika la Taifa la Utangazaji (TBC) alipotembelea kwa ajili ya hafla ya Kukabidhi na kuzindua gari la kurushia matangazo (OB Van) lililotolewa kwa Msaada wa Serikali ya China jana jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Li Yunchao akisalimiana na baadhi ya Wafanyakazi wa Startimes na TBC mara baada ya kuwasili katika Viwanja vya Ofisi za Shirika la Taifa la Utangazaji (TBC) alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya Kukabidhi na kuzindua gari la kurushia matangazo (OB Van) leo jijini Dar es Salaam.Gari hilo limetolewa kwa Msaada wa Serikali ya China.Katikati ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wa Tanzania Dkt. Fenella Mukangara.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akijadiliana na jambp na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga, katikati ni Mwakilishi wa Kampuni ya Startimes Bw. Jack Zhou.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene (katikati) wakati wa hafla ya makabidhiano na uzinduzi wa Gari la kisasa la kurushia matangazo ya moja kwa moja (OB Van) ambalo Serikali ya China ili kutoa msaada kwa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC). Kushoto ni Mkurugenzi wa TBC Bw. Clement Mshana.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akitoa hotuba wakati wa hafla fupi ya makabidhiano na uzinduzi wa gari la kurushia matangazo(OB Van) la Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) leo katika viwanja vya TBC jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara( wa pili kutoka kushoto) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa matumizi ya Gari la kurushia matangazo la TBC, kutoka kulia ni Makamu Waziri wa Biashara wa Jamhuri ya watu wa China Li Jingzao, Makamu wa Rais wa China Li Yunchao na wa mwisho kushoto ni Mkurugenzi wa TBC Bw. Clement Mshana
Gari la kisasa la kurushia matangazo ya moja kwa moja lililokabidhiwa kwa TBC likiwa katika viwanja vya Shirika hilo Mikocheni jijini Dar es Salaam
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akikagua ndani ya Gari la kisasa la kurushia matangazo la TBC mara baada ya uzinduzi wake leo jijini Dar es Salaam.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment