Friday, 25 April 2014

SAFI SANA: CHINA YAZIFUNGUA TOVUTI 110 ZINAZOONESHA MASUALA YA NGONO



China imezifungia tovuti 110 ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kitaifa ya kuzuia masuala ya ngono kwenye mitandao.


Imeeleza taarifa ya serikali hiyo inayosimamia masuala ya taarifa mitandao iliyotolewa juma hili.



Mitandao ya kijamii 3,300 inayotoa huduma nchini China ,ikiwemo WeChat na Sina Weibo na majukwaa ya kijamii kwenye mitandao yameondolewa katika kampeni iitwayo
 "Cleaning the Web 2014".


 Karibu matangazo  7,000 na ujumbe wa maneno 200,000 wenye aina za maneno ya ngono vimeondolewa.

Kampeni hiyo ni sehemu ya utaratibu wa kuondoa usambaaji wa mitandao ya ngono katika nchi hiyo ambayo hadi kufikia mwezi disemba 2013 ilikuwa na watumiaji wa intaneti wapatao milioni618,ambapo mwaka 2012 ilizifungia blog 97,000 kutokana na kujihusisha na uandikaji wa habari za ngono

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!