Wednesday 11 December 2013

YALIYOJIRI KATIKA MSIBA WA MADIBA ....VIONGOZI MBALIMBALI DUNIANI WAHUDHURIA IBADA MAALUM YA KUMUOMBEA MZEE MANDELA LEO



Rais wa Marekani,Barack Obama akihutubia maelfu wa waombolezaji wa Msiba wa Rais wa Zamani wa Afrika Kusini, Hayati Nelson Mandela waliopo kwenye Uwanja wa FNB Soccer City,Jijini Johannesburg.Rais Obama amemsifia sana Mzee Mandela na kwa mengi aliyoyafanya kwa Waafrika Kusini na Dunia nzima kwa Ujumla.


 Familia ya Hayati Nelson Mandela ikifuatilia misa maalum ya kumuombea kiongozi huyo Maarufu Duniani pamoja na kwamba mvua kubwa iliyokuwa ikinyesha.




 Maelfu wa wananchi wa Afrika Kusini wakiwa wamefurika kwenye Uwanja wa FNB Soccer City,Jijini Johannesburg
Rais wa Marekani,Barack Obama na Mkewe wakiwa kwenye misa hiyo.
kwa picha zaidi bofya soma zaidi
Mke wa zamani wa Hayati Mzee Nelson Mandela, Winnie Madikizela-Mandela akionekana ni mwenye huzuni mkubwa wakati wa ibada maalum iliyofanyika leo kwenye Uwanja wa FNB Soccer City,Jijini Johannesburg.
 Mke wa zamani wa Hayati Mzee Nelson Mandela, Winnie Madikizela-Mandela (kushoto) na mjane wa sasa wa Mzee Mandela,Mama Graca Machel ( kulia mwisho ) wakifuatilia misa hiyo.
 Maelfu wa wananchi walijitokeza katika misa hiyo pamoja na mvua kubwa kunyesha muda mrefu

Wakuu wa nchi mbali mbali Duniani wakiwa kwenye Misa hiyo leo.ambapo Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ni mmoja wa viongozi waliopata fursa ya kuhudhuria misa hii.
 Mmoja wa wananchi wa Afrika Kusini akinyoosha mkuno juu kuonyesha ishara ushindi

PICHA KWA HISANI YA PAMOJA BLOG.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!