Meneja wa Kampuni inayojishughulisha na kurusha matangazo yanayohusu ligi ya mpira wa miguu ya Tanzania kupitia mtandao, Nzowa Wawila akizungumza juu ya umuhimu wa mtandao huo wakati wa kutoa msaada kwa watoto yatima kituo cha Amani Nsagala Uyole.
Baadhi ya watoto katika kituo cha Kulelea yatima cha Aman Nsagala uyole wakimsikiliza kwa makini Meneja wa Kampuni inayojishughulisha na kurusha matangazo yanayohusu ligi ya mpira wa miguu ya Tanzania kupitia mtandao, Nzowa Wawila
Baadhi ya watoto katika kituo cha watoto yatima cha Aman Nsagala wakiimba Nyimbo kabla ya kukabidhiwa msaada huo.
Meneja wa Kampuni inayojishughulisha na kurusha matangazo yanayohusu ligi ya mpira wa miguu ya Tanzania kupitia mtandao, Nzowa Wawila kushoto akikabidhi msaada wenye thamani ya Tsh 1,500,000 katika kituo kituo cha kulelea watoto yatima cha Amani
Hili ni eneo ambalo watoto hawa hukutania na kujifunza mambo kadha wa kadha
Msimamizi Msaidizi wa Kituo hicho kilicho chini ya Idara ya Wanawake ya Kanisa la Moraviani, Isabela Haonga akitoa neno la Shukurani kwa kampuni ya LAJANN E-SYSTEM ENTERPRISES kwa msaada uliotolewa kwa watoto yatima
Meneja wa Kampuni inayojishughulisha na kurusha matangazo yanayohusu ligi ya mpira wa miguu ya Tanzania kupitia mtandao, Nzowa Wawila akiwa katika picha ya pamoja na watoto yatima wa kituo cha Aman Nsagala Uyole.
********
JAMII imetakiwa kuisaidia Serikali katika kuifichua na kuziba mianya inayosababisha Watoto wa mitaani na wanaoishi katika mazingira magumu kuzidiu kuongezeka licha ya Asasi nyingi kujitokeza kuwahudumia.
Mwito huo ulitolewa wa na Katibu Mkuu wa Jimbo la Kusini Magharibi la Kanisa la Moraviani Tanzania, Mchungaji Willy Mwasile, wakati akipokea msaada kutoka kwa kampuni ya LAJANN E- System Enteprises ya Jijini Dar Es Salaam kwa ajili ya kituo cha kulelea watoto Yatima cha Aman Nsalaga kilichopo Uyole Jijii Mbeya.
Mchungaji Mwasile alisema ni vema utafiti ukafanyika ili kubaini chanzo cha ongezeko la Yatima mitaani ili liweze kudhibitiwa na kuondolewa kabisa kwa kudhibiti ndoa zisizo halali kwa wale wanaobeba mimba kiholela na kutokuwa na uwezo wa kulea.
Akitoa msaada huo Meneja wa Kampuni hiyo inayojishughulisha na kurusha matangazo yanayohusu ligi ya mpira wa miguu ya Tanzania kupitia mtandao huu www.ligikuu.co.tz , Nzowa Wawila, alisema kutokana na kukaribia kufunguliwa kwqa pazia la Ligi kuu wameona ni vema wakatoa msaada kwa jamii ili kutambua umuhimu wao.
No comments:
Post a Comment