Thursday 4 July 2013

BOMOA BOMOA YA POMBE MAGUFULI YAANZA.....JENGO LA BUSINESS PARK ( GREEN ACRES ) LABOMOLEWA

 
 
 
 
 
 Baada Waziri wa Ujenzi, Pombe Magufuli kutoa maagizo kwa wenye majengo yaliyo pembezoni mwa barabara ya Ali Hassan Mwinyi, kubomoa wenyewe majengo yao ili kupisha upanuzi wa barabara hiyo, kuonekana yakisua sua, hatimaye leo ameanza rasmi kazi ya kubomoa kwa Greda katika majengo ya wale walioonekana kukaidi agizo hilo. 


Katika kutekeleza agizo hilo zoezi hilo limeanzia kwenye Jengo la Business Park (Green Acres) lililopo eneo la Victoria ambapo hadi hivi sasa zoezi hilo bado linaendelea pande hizo chini ya usimamizi ya Askari
 
 Msongamano pande hizo.....
 Tayari ukuta ukiwa umeshashushwa chini wa upande wa barabarani  huku baadhi ya watu wanaofanya shughuli zao katika jengo hilo wakihaha kuhamisha baadhi ya vifaa.
 Katapila likiendelea na kazi ya kubomoa hapa ni jengo la pili lililokaribu na Green Acres nalo likiliwa hapa tayari ukuta ukiwa unashushwa.....
Katapila likiendea kusambaratisha kuta hizo.....

Sufianmafoto

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!