Friday 24 May 2013

KIJANA ALIYEJULIKANA KAMA RAMA MLA WATU APELEKWA HOSPITALI YA VICHAA DODOMA, MAMA YAKE AACHIWA HURU, YADAIWA ALIUWA BILA KUKUSUDIA.

Mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam imeamua kumuachia huru Ramadhani Selemani Mussa ambaye alikuwa akikabiliwa na kesi ya kukutwa na kichwa cha mtoto aliyejulikana kwa jina la Salome(3) mnamo Apil 25. Kijana huyo(RAMADHAN) ambaye muda wote huo alikuwa rumande katika gereza la Segerea akisubiri hukumu yake ya mauwaji, alikamatwa hospitali ya Muhimbili mwaka 2008.

Baada ya Mahojiano Rama alikiri kuwa alikuwa na tabia ya kula nyama za watu na kwamba ni tabia ambayo amefundishwa kichawi toka alipokuwa mdogo. Mahakama imemuachia huru kwasababu mtuhumiwa alitenda kosa hilo pasipo kuwa na akili timamu. Hata hivyo mahakama hiyo imetoa agizo la kuendelea kumuweka kijana huyo katika hospitali ya wagonjwa wenye matatizo ya akili iliyopo Dodoma. k mama wa Kijana  huyo (Bi Khadija Ally) ambaye pia alikuwa rumande kufuatia tuhuma hizo, aliachiwa huru. Rama amepelekwa hospitali ya Isanga iliyopo Dodoma mpaka pale atakapona.




Ramadhani akiwa na mama yake mzazi, Khadija Ally wakielekea mahakamani.
Kijana Ramadhani akihojiwa.



Mama wa Marehemu Salome akilia kwa uchungu wakati wa mazishi ya mwanae.




Kijana Ramadhani akiwa na mama yake mzazi.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!