Sunday 21 April 2013
USAFIRI WA TRENI JIJINI KUANZA TENA SAFARI ZAKE KESHO APRIL 22
Huduma za usafiri wa treni jijini zitaanza tena kesho, baada ya huduma hizo kusimamishwa kwa muda kutokana na ukarabati katika tuta la reli huko Tabata mwananchi, ambalo lilikuwa limeharibika kutokana na nvua zinazoendelea kunyesha. na kwamba huduma hizo za usafiri zitaanza saa 12.30 za asubuhi katika kituo cha ubungo maziwa mpaka kituo cha reli, na huduma hiyo ya kwanza itamalizika saa 5 asubuhi.
Huduma ya pili itaanza saa10, toka kituo cha reli kwenda Ubungo maziwa,kupitia vituo vya Buguruni kwa mnyamani ,Tabata, Kamata, Bakhresa, Tabata matumbi, Tabata mwananchi,Mabibo, na huduma hizo za usafiri zitamalizika saa 4 usiku.
Taarifa kwa niaba ya michuzi blog.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment