Tawi la chama cha mapinduzi nchini Uingereza limetoa salamu kwa aidha kwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dr.Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohammed Shein, kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,na kwa WaTanzania wote kwa ujumla kwa kutimiza miaka 49 ya Muungano wa nchi yetu, TANZANIA.
Aidha chama hicho kimewasihi watanzania kuendelea kuulinda Muungano wetu kwa kudumisha AMANI, UPENDO, UMOJA, UTULIVU na MSHIKAMANO, kwani hizo ndizo silaha zilizoweza kuulinda Muungano huu ambao umetuletea Heshima ya kipekee Duniani kote, kwa nusu karne sasa.
Katika salamu hizo wana CCM nchini Uk wamesisitiza kuwa tujifunze kutoka nchi mbalimbali duniani ambazo wamechezea amani yao na sasa wamo ndani ya dimbwi kubwa la machafuko, mauaji ya halaiki na yanayoendelea kila kukicha. Maelfu ya raia wasio na hatia wamepoteza maisha yao katika Nchi mbalimbali, wengine kupata ulemavu wa kudumu, kupoteza makazi na kuharibikiwa na mwenendo mzima wa mfumo wa maisha yao, milipuko ya mabomu isiyoisha na raia kukosa amani na utulivu. WaTanzania kamwe tusikubali kuipoteza amani yetu kwa uchochezi wa watu wachache, na ambao kwa sababu zao binafsi hawatutakii mema , na mpaka wako tayari kutumia visingizio kama vya siasa na dini ili watusambaratishe.
Mariam A. Mungula
KATIBU
CHAMA CHA MAPINDUZI – UINGEREZA
No comments:
Post a Comment