Tuesday 30 April 2013

UHOLANZI YAPATA MFALME MPYA

Malkia Beatrix wa Uholanzi amesaini kanuni ya kumpa kiti mwanawe Willem Alexander, Mfalme wa kwanza wa nchi hiyo kwa zaidi ya miaka 100. Umati wa Watu ulimiminika asubuhi ya leo mjini Amsterdam kushuhudia sherehe hiyo.
Malkia Beatrix , mwenye haiba ya kupendwa na wengi amemaliza utawala wake wa miaka 33 leo, katika sherehe iliyotangazwa moja kwa moja na Televisheni na utiaji saini wa kumkabidhi Ufalme mwanawe wa kiume kushuhudiwa na maelfu ya Waholanzi waliovalia sare za rangi ya machungwa. Pia sherehe hiyo imeshuhudiwa na mamilioni ya watazamaji kwa njia ya Televisheni.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!