Monday 23 July 2018

WATANO WAHUKUMIWA KUNYONGWA KWA MAUAJI YA BILIONEA MSUYA

Mahakama Kuu ya Tanzania imewahukumu kunyongwa hadi kufa washitakiwa watano baada ya kuwatia hatiani kwa kumuua kwa makusudi mfanyabiashara wa Arusha na Mirerani, Erasto Msuya.

Waliohukumiwa adhabu hiyo ni mshtakiwa wa kwanza, Sharifu Mohamed, mshtakiwa wa tatu, Mussa Mangu, wa tano, Karim Kuhundwa, wa sita Sadick Mohamed na wa saba; Ally Mussa Majeshi.
Hukumu hiyo imetolewa leo na Jaji Salma Maghimbi aliyesikiliza kesi hiyo.
Pia, Mahakama imemwachia huru mshtakiwa wa pili, Shwaibu Jumanne baada ya kukosekana ushahidi dhidi yake.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!