Thursday 17 May 2018

Imethibitika Ebola imeenea DR Congo mjini

Leo May 17, 2018 Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo hii leo imethibitisha kuwa ugonjwa wa ebola umeenea mpaka mjini.

Waziri wa Afya nchini humo Oly Ilunga amesema kuwa mlipuko wa maradhi hatari ya Ebola nchini humo umechukua sura mpya huku wataalamu wa afya wakifanya juhudi kuwatambua watu ambao wamekuwa karibu na wale waliothibitishwa kuwa na maambukizi ya ugonjwa huo.
Inaaminika kuwa mlipuko mpya wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambao ulianzia katika jimbo la Equateur tayari umeuwa watu zaidi ya 32.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!