Wednesday 4 April 2018

Taratibu za kuurejesha mwili wa aliyeuawa London zaendelea

Arusha. Juhudi za kuchangisha fedha kwa ajili ya kuusafirisha mwili wa Mtanzania aliyeuawa Uingereza, Leyla Mtumwa zinaendelea nchini humo.



Taarifa zilizopatikana zinaeleza kuwa tayari kitengo cha polisi cha uchunguzi wa mauaji hayo, kimeshakamilisha uchunguzi wao na sasa zinasubiriwa taratibu nyingine za kuruhusu mwili huo kurejeshwa nchini.
“Michango inaendelea vizuri, kila kitu kipo sawa, uhakika wa kumrudisha Tanzania upo, lakini bado taratibu ndogo ndogo tu, na tutawajuza.” Kimesema chanzo kimoja kutoka nchini humo.
Leyla, anadaiwa kuchomwa visu hadi kufa na mumewe, siku wa kuamkia Machi 29 huko eneo la Tottenham, Uingereza.
Leyla ni mtoto wa Hidaya Mtumwa, mwanamke aliyewahi kutungiwa wimbo na mwanamuziki Pepe Kalee, miaka 1990.

MWANANCHI.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!