Saturday 3 October 2015

NDEGE ZA URUSI ZAFANYA MASHAMBULIO NCHINI SYRIA


Image copyrightAFP
Image captionSyria

Ndege za Urusi zimefanya mashambulio zaidi nchini Syria.


Msemaji wa jeshi la Urusi, alieleza kuwa ndege zao zimefanya mashambulio 20 katika siku iliyopita, na kupiga maeneo kadha ya IS.

Image copyrightRIA NOVOSTI
Image captionSyria

Lakini waziri wa ulinzi wa Uingereza, Michael Fallon amesema, katika mashambulio 20 yaliyofanywa na ndege za Urusi, moja tu lililenga IS.
Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron ,amerudia tena matamshi yake ya kuikosoa Urusi akidai kuwa inaunga mkono uongozi wa rais Assad aliyemtaja kuwa muuaji.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!