Ratiba ya kusafirisha mwili wa marehemu Mhe. Capt. John Komba itakuwa kama ifuatavyo:
Tarehe 02/3/2015 saa 1 asubuhi misa parokia ya Mt. Bikira Maria Mpalizwa iliopo mbezi , saa 4 asubuhi mwili utaelekea Karimjee kwa ajili ya kuagwa, na saa 8 mchana mwili utaelekea airport tayari kwa safari ya Songea.
Mazishi yatafanyika tarehe 3/3/2015 kijijini kwake Lituhi.
Kufuatia Msiba huu shughuli za kamati hazitakuwepo kwa kesho tarehe 2/3/2015. Ukipata taarifa hii tafadhali mjulishe na mwingine.
IMETOLEWA NA;
OFISI KATIBU WA BUNGE
1.3.2015
NA. |
MUDA
| TUKIO | MHUSIKA | |
1.
| 12:00 - 01:00 | Familia na Waombolezaji kupata chai nyumbani | Kaimu Katibu wa Bunge | |
2.
| 01:00 - 04:00 | Misa ya kuaga mwili wa Marehemu | Kanisa Katoliki,Parokia ya Bikira Maria Mpalizwa | |
3.
| 04:00 - 04:30 | ·Ndugu, Jamaa na Wananchi kuwasili katika Viwanja vya Karimjee ·Viongozi wa Vyama vya Siasa, Waheshimiwa Wabunge, Manaibu Waziri, Mawaziri kuwasili na kuketi katika nafasi zao | Katibu wa Bunge | |
4.
| 04:33 | Kiongozi wa Upinzani Bungeni kuwasili | Kaimu Katibu wa Bunge | |
5.
| 04:36 | Mhe. Naibu Spika kuwasili | Kaimu Katibu wa Bunge | |
6.
| 04:39 | Mhe. Spika kuwasili | Mhe. Naibu Spika | |
7.
| 04:42 | Mhe. Waziri Mkuu kuwasili | Mhe. Spika | |
8.
| 04:50 | Mhe. Makamu wa Rais kuwasili | Mhe. Spika | |
9.
| 05:00 | Mhe. Rais kuwasili | Mhe. Spika | |
10.
| 05:00 | Mwili wa Marehemu kuwasili kwa gwaride maalum la Sergeant-At-Arms | Katibu wa Bunge | |
11.
| 05:00 - 05:15 | Sala fupi | Kanisa Katoliki,Parokia ya Bikira Maria Mpalizwa | |
12.
| 05:15 - 05:20 | Wasifu wa Marehemu | Kaimu Katibu wa Bunge | |
13.
| 05:20 - 05:30 | Salamu na Rambirambi za Chama cha Mapinduzi (CCM) | Katibu Mkuu, CCM | |
14.
| 05:30 - 05:35 | Salamu na Rambirambi kutoka kwa Kiongozi wa Upinzani Bungeni | Kiongozi wa Upinzani Bungeni | |
15.
| 05:35 - 05:45 | Salamu na Rambirambi za Serikali | Waziri Mkuu | |
16.
| 05:45 - 05:55 | Salamu na Rambirambi za Uongozi wa Bunge | Mhe. Spika | |
17.
| 05:55 - 06:00 | Neno la Shukrani toka kwa familia | Mwakilishi wa Familia | |
18.
| 06:00 - 06:15 | Utaratibu wa safari | Kaimu Katibu wa Bunge | |
19.
| 06:15 - 07:15 | Kuaga Mwili wa Marehemu kulingana na Itifaki | MC | |
20.
| 07:15 | Mwili wa Marehemu kuondoka uwanjani kuelekea Uwanja wa Ndege | MC | |
21.
| 07:20 - 07:25 | Viongozi wa Kitaifa kuondoka kulingana na Itifaki | MC | |
22.
| 07:40 | Mwili wa Marehemu kuwasili Uwanja wa Ndege | Kaimu Katibu wa Bunge | |
23.
| 08:00 | Mwili, Familia na Waombolezaji kuondoka kuelekea Songea | Kaimu Katibu wa Bunge | |
24.
| 10:00 | Mwili wa Marehemu kuwasili Uwanja wa Ndge Songea na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa | Ofisi ya Mkuu wa Mkoa | |
25.
| 10:00 - 10:15 | Mwili wa Marehemu kuelekea Uwanja wa Majimaji | Ofisi ya Mkuu wa Mkoa | |
26.
| 10:15 - 11:00 | Mkuu wa Mkoa kuongoza wakazi wa Ruvuma kuaga mwili wa Marehemu | Ofisi ya Mkuu wa Mkoa | |
27.
| 11:00 - 01:00 | Mwili wa Marehemu kuondoka Uwanja wa Majimaji kuelekea Lituhi, Nyasa | ·Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ·Kaimu Katibu wa Bunge | |
28.
| 01:00 | Mwili kuwasili nyumbani na taratibu za kifamilia kuendelea | MC |
No comments:
Post a Comment