Thursday 18 December 2014
MWANAUME MTANZANIA ALIYEUA WATOTO WAKE WAWILI NCHINI AUSTRALIA AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA
Charles Mihayo (36) mzaliwa wa Tanzania ambaye mwezi wa April 20 mwaka 2014 aliwaua watoto wake wawili wa kike huko nyumbani kwake Melbone Australia amehukumiwa kifungo cha maisha.
Taarifa zinadai kuwa baada ya Charles kuachwa na mke wake hasira zilimpanda bwana Mihayo na kuamua kufanya ukatili kwa watoto wake mwenyewe Savannah( 4)na Indiana (3) alifanya hivyo kwa lengo la kumuumiza mke wake kwa lengo la kulipiza kisasi.
Inadaiwa kuwa aliwaua na kwa kuwakandamiza na mto baada ya kucheza nao.
Taarifa hizo zinaeleza pia kuwa siku ya mauaji hayo yalipofanyika, mama wa watoto hao aliwapeleka kwa baba yao bwana Mihayo, na baada ya kufika baba huyo aliwafanyia shopping ya nguo na viatu vipya kabla hajawaua.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
1 comment:
Kukaa nje sana kunaharibu akili,huyo jamaa akapimwe akili zake tayari ni sita kasorobo,mgonjwa huyo.
Post a Comment