Friday 31 October 2014

TUTASHIRIKIANA NA WAPENDA AMANI KUISAIDIA DRC KUWA NA AMANI-TANZANIA



Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Ramadhan Mwinyi akizungumza wakati wa Mkutano wa Kamati ya Nne ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa iliyokuwa ikijadili ajenda kuhusu tathmini ya jumla ya Operesheni za Ulinzi wa Amani za Umoja wa Mataifa. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kati ya nchi zinazochangia wanajeshi wake katika operesheni hizo za ulinzi wa amani.




Sehemu ya wajumbe wa Kamati ya Nne ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, wakifuatilia majadiliano ya ajenda kuhusu Operesheni za Ulinzi wa Amani za Umoja wa Mataifa.



Na Mwandishi Maalum, New York
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  imeihakikishia  Jumuiya ya Kimataifa  ya kuwa itaendelea  kushirikiana na wapenda  amani katika kuisaidia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ( DRC)  kuwa  na amani na usalama.

Akichangia majadiliano  juu ya ajenda inayohusu  tathimini  ya  jumla  ya Operesheni za Ulinzi wa Amani  chini ya Umoja wa Mataifa.  Naibu Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Ramadhan Mwinyi amesema, Tanzania inafanya hivyo kwa kutambua wajibu wake katika  medani  ujenzi wa amani ya Kimataifa.

Amesema  pia  kuwa, ni kwa kutambua wajibu huo ,ndiyo sababu iliyoifanya Serikali ya Jamuhuri ya Muungano  wa Tanzania kufikia makubaliano na nchi  wanachama wenzie  katika SADC na  Maziwa  Mkuu  ( ICGLR), kujitolea  kupeleka wanajeshi wake huko  DRC ili  kuunga   mkono juhudi za kuwasaidia wananchi wa  DRC kuwa na amani , usalama  na maisha  yenye uhakika.

Balozi Mwinyi amesema  kuwa Tanzania inajivunia  kuwa  wanajeshi wake  wanaohudumu kupitia FIB   ambayo ni sehemu ya     MONUSCO  licha ya  mazingira magumu na hatari wanayokabiliana nayo wameonyesha  umahiri  mkubwa  ikiwa ni pamoja na kujitoa muhanga maisha yao kuwalinda raia wasiokuwa na hatia DRC  pamoja na kurejesha amani na  usalama.

No comments:

 

ADVERTISE WITH US

AFRICAN FASHION

PLACE YOUR ADS HERE!