Saturday 28 December 2013
WABUNGE WAJISALIMISHA MADAWA YA KULEVYA
Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kipentekoste, William Mwamalanga
Baada ya tishio la kupelekwa kwenye Mahakama ya Kimataifa ya ICC, watu watano wakiwemo wabunge watatu wa CCM wanaodaiwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya wamejisalimisha kwenye kamati ya kidini inayojihusisha na maadili nje na ndani ya makanisa.
Baada ya tishio la kupelekwa kwenye Mahakama ya Kimataifa ya ICC, watu watano wakiwemo wabunge watatu wa CCM wanaodaiwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya wamejisalimisha kwenye kamati ya kidini inayojihusisha na maadili nje na ndani ya makanisa.
JACKIE CLIFF, ATUMA UJUMBE MZITO KWA MARTIN KADINDA..KUFUATIA YALIYOMKUTA CHINA.....
Yaelekea mwanadada Jackie alikuwa amejipanga kisawa sawa na alijitoa muhanga na kujua lolote lingeweza kumpata kutokana na kazi aliyo kuwa akifanya ya kubeba sembe. Jackie alijipanga na
kuamua kumuachia rafiki yake kipenzi Martin Kadinda maagizo na wosia wake just incase ikatokea akafariki. Jackie aliweza kuandika ujumbe huo kwenye status yake ya BBM kama inavyo onekana hapa chini.
ASILIMIA 96 YA WANAFUNZI WALIOFAULI DARASA LA SABA KUJIUNGA NA SEKONDARI ZA SERIKALI
ASILIMIA 96.15 ya wanafunzi wa darasa la saba waliofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka huu na kufaulu, ndio waliochaguliwa kujiunga na sekondari za serikali.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu –TAMISEMI, Jumanne Sagini aliwaambia waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kwamba jumla ya wanafunzi 411,127 kati ya 427,609 waliofaulu mtihani huo ndio watakaoanza kidato cha kwanza mwakani.
Friday 27 December 2013
OPERATION TOKOMEZA...HII NI SABABU MOJAWAPO ILIYOSABABISHA BAADHI YA MAWAZIRI KUFUKUZWA....
Like Sabibo Camp like Operesheni Tokomeza. Na hii ni just a drop of ice berg...
Hivi unaweza kujiuliza kwenye hizo kambi vingapi hatujavijua vilifanyika? Kama hadi sasa, kwa mujibu wa taarifa ya kamati wanaume walilazimishwa kufanya mapenzi na miti hadi wamalize haja zao na mengine mengi....
TASWIRA KATIKA MAZISHI YA MWANAFUNZI WA CBE ZEINABU J KASENGA ALIYEFARIKI JUZI DEC 23:
MWANADADA JACKIE CLIFF(VIDEO QUEEN) ADAIWA KUKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA NCHINI CHINA
Mwanamke wa Kitanzania mwenye umri wa miaka 28 amekamatwa na kilo 1.1 za dawa za kulevya aina ya heroin huko Macao. Dawa hizo zilikutwa tumboni mwake baada ya kushtukiwa na kufanyiwa X-ray ambapo alikutwa na jumla ya vidonge 66 vyenye thamani ya dola za Kimarekani 137,720.
Kwa mujibu wa mtandao wa China Daily ambao hata hivyo haukujata jina la mrembo huyo, mwanamke huyo alikuwa akisafiri kutoka Thailand akielekea Macao Jumanne iliyopita. Aliwaambia polisi kuwa alikuwa anaelekea Guangzhou ambao ni mji wa jimbo la Guangdong huko China.
Pichani ni mwanamke huyo wa Kitanzania (akiwa amefunikwa uso) aliyekamatwa na kilo 1.1 za heroin huko Macau. Hapo amepigwa picha na vidonge vyake kwenye press conference huko Macau, Disemba 19, 2013.
Licha ya habari kushindwa kubainisha mwanamke huyo ni nani, baadhi ya wachunguzi wa mambo toka kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii waliweza kubaini kuwa inawezekana mwanadada huyo akawa ni Jackie Cliff kutokana na sababu zao binafsi wanaouzijua wao na pia ikizingiatiwa kuwa mwanadada huyo alikuwa nchini China kwa muda mrefu akizunguka kwenye mitaa na majimbo mbalimbali ya nchi hiyo yaliyotajwa kwenye habari hiyo.
MAWAZIRI WALIOFUTWA KAZI WATOA YA MOYONI
BAADA ya Rais Jakaya Kikwete kutengua uteuzi wa mawaziri watatu na mmoja kujiuzulu, kutokana na kashfa zilizotokana na Operesheni Tokomeza Ujangili, viongozi hao wamezungumza yaliyowasibu kila mmoja kwa staili yake.
Thursday 26 December 2013
BINTI MWENYE SURA YA KIUME AZUNGUMZIA CHANGAMOTO ANAZOKUTANA NAZO..
Queen ni mtoto wa 4 kati yya familia ya watoto 5. Ni msichana mzuri
na mrembo kimtazamo, lakni tatizo kubwa linalomkabili maishani mwake ni
nywele ambazo zimekuwa zikimfanya aonekane kama mwanaume…..
Akiongea kwa njia ya mtandao, Queen amesimulia kuhusu changamoto anazokumbana nazo kutokana na tatizo hilo.
“Nimerithi hizi nywele toka kwa mama yangu na zilinianza nikiwa na
miaka 21. Kadri miaka ilivyozidi kusonga mbele, tatizo hili lilizidi
kusambaa mwili mzima.
DIAMOND KUWASOMESHA WATOTO WATATU WALIOWEZA KUCHEZA NGOLOLO
Mmoja ya watoto watatu walioshinda kucheza ngololo.management yangu ya WCB itawasomesha miaka yote waliyobakiza shuleni ikiwa ni pamoja na kuwahamishia katika shule zilizo bora zaidi....Ahsanten sana Daresalaam kwa sapoti mliyonipa jana ....
WENGI WAJITOKEZA KUUAGA MWILI WA KOCHA WA MAKIPA WA WA SIMBA MAREHEMU JAMES KISAKA LEO
Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Kocha wa makipa wa Simba, marehemu James Kisaka likiingizwa kwenye basi la klabu hiyo, baada ya kutolewa heshima za mwisho katika misa iliyofanyika katika Kanisa la Muhimbili, Dar es Salaam. Marehemu Kisaka atasafirishwa kwenda kwao wilayani Muheza, Tanga kwa mazishi yatakayofanyika kesho.
DIAMOND NA WEMA SEPETU WA "SEPETUNGA"
Diamond Platnumz na Wema Sepetu wameendelea kuliimarisha penzi lao kadri siku zinavyoenda. Uhakika wa kuwa wapenzi hawa wenye uhusiano wa ‘on and off’ wamerudiana kwa kasi, ulijulikana baada ya picha zao wakiwa Hong Kong kusambaa mtandaoni hali iliyopelekea kuzuka mgogoro mkubwa kati ya Diamond na mpenzi wake Penny ambaye kuna tetesi kuwa wameshaachana rasmi
TANGA WATAHADHARISHWA KUHUSU KUWEPO KWA KIMBUNGA
ASKOFU AWALIPUA WABADHIRIFU KATIKA IBADA YA KRISMAS
WALAJI WA KITI MOTO (NGURUWE) WANAHATARI YA KUPATA KIFAFA.
CHUO Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimehadharisha walaji wa nyama ya nguruwe nchini, kuwa wanakabiliwa na hatari ya kupata kifafa.
Wednesday 25 December 2013
MAITI YAKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA MOROGORO
Maiti ikiwa ndani ya gari yenye namba ya usajili T 887 BSW eneo la chumba cha kuhifadhia maiti cha hospotali kuu ya mkoa wa Morogoro, baada ya gari hilo kukamatwa majira ya saa 7 usiku eneo la Mikumi,likiwa na watu watatu na maiti ya binadamu inayodaiwa kupoteza maisha baada ya kumeza kete hizo za zinazodaiwa kuwa ni madawa ya kulevya.
PICHA NA JUMA MTANDA
PICHA NA JUMA MTANDA
KOCHA WA ZAMANI WA SIMBA AFARIKI DUNIA
James Kisaka enzi za uhai wake.
Aliyekuwa kocha wa makipa wa Klabu ya Simba, James Kisaka amefariki dunia leo asubuhi katika Hospitali ya Burhan, Dar es Salaam. Kisaka aliyewahi kuwa kipa wa timu hiyo miaka ya nyuma, alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya kichwa, macho na miguu kwa muda mrefu.
MUNGU AIPUMZISHE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI. AMINA
GPL.
WATANZANIA KUANZA MWAKA MPYA 2014 KWA MAUMIVU BAADA YA TANESCO KUPANDISHA BEI ZA UMEME KUANZIA JANUARI MOSI.
WATANZANIA wataanza Mwaka Mpya 2014 kwa maumivu, baada ya Shirika la Umeme (TANESCO) kuidhinishiwa kupandisha bei za umeme kuanzia Januari mosi.
Tuesday 24 December 2013
JK ATOA ZAWADI YA XMAS KW A WATOTO YATIMA NA WAZEE WASIOJIWEZA
Na Kiza Sungura-MAELEZO,Dar es salaam
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Dkt Jakaya Mrisho kikwete ametoa jumla ya kilo za mchele 1,200 , lita 220 za mafuta na mbuzi 25 kwa ajili ya zawadi ya sikukuu ya Krismas kwa makundi maalum.
Zawadi hizo zilikabidhiwa jana (leo) na Kaimu Kamishna wa Ustawi wa Jamii Bibi Beatrice Fungamo kwa niaba ya Rais Kikwete kwenye sherehe fupi iliyofanyika katika Uwanja wa Mahabusu ya Watoto jijini Dar es salaam.
JUST IN.......VURUGU KURASIN TEMEKE!!
Mali zimeharibiwa na kuvunjwa kwa Maghala na huku risasi zinarindima kama maji sasa hivi Kurasini Temeke, ......................stay tuned for more info!!!
Credit:williammalecela.blogspot.com
MKE WA BILLIONEA ALIYEJIUA KWA RISASI JIJINI DAR AIBUA MAZITO
MKE wa marehemu bilionea Suleiman Muhema, Zihija Muhema ametoboa siri kuhusiana na kifo cha mume wake aliyekutwa amefariki dunia kwa kujipiga risasi akiwa ndani ya gari lake Kisarawe, Pwani.
Akizungumza na paparazi wetu juzi, Zihija alisema kifo cha mume wake kimegubikwa na usiri mkubwa baada ya mumewe siku ya tukio kumwambia kuwa anamfuata mama yake aliko, hali ambayo ilimshitua kwa kuwa mama yake mzazi alishafariki siku nyingi zilizopita.
Monday 23 December 2013
AUAWA KWA TUHUMA ZA UCHAWI JIJINI DAR... JAMANI KESI KAMA HIZI ACHENI POLISI WAFANYE KAZI YAO! HUENDA HATA NI MGONJWA WA AKILI...
WANANCHI wenye hasira kali wamempiga hadi kumuua mtu mmoja mwanaume aliyesadikiwa kuwa ni mchawi baada ya kuanguka akiwa amepanda ungo maeneo ya Mbezi Luis jijini Dar es Salaam, Mtanzania limeshuhudia.
Kijana huyo mkazi wa Mwanza anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 20 hadi 25, alianguka jana saa 12 asubuhi maeneo hayo baada ya kudai kuwa alikuwa kwenye safari zake za kishirikina.
Kabla ya kufariki alisema “mimi nilikuwa na wenzangu sita,
wanaume watatu na wanawake watatu ambapo tulikuwa tunatoka Mwanza kuelekea kwenye mkutano wetu”
wanaume watatu na wanawake watatu ambapo tulikuwa tunatoka Mwanza kuelekea kwenye mkutano wetu”
“Lakini mimi kwa bahati mbaya nilikiuka masharti tuliyopewa na mkuu kwa kufungua macho ndipo ghafla nilianguka na kupata kadhia hii inayopelekea mauti yangu”
Hata hivyo kutokana na vurugu zilizokuwapo eneo hilo la tukio, ambapo wananchi wa eneo hilo walikuwa wanataka kumuua, kijana huyo alishindwa hata kutaja jina lake kutokana na kipigo alichokuwa anakipata kutoka kwao.
MSANII ALIYEGEUKA KUWA MGANGA WA KIENYEJI
HAYA JAMANI NAFASI ZA KAZI HIZO!
Secretary
Turkish Embassy
Email Address: Click to Email
Phone: No Phone Calls
Area: Dar Es Salaam
Application Deadline: Jan 08, 2014
Phone: No Phone Calls
Area: Dar Es Salaam
Application Deadline: Jan 08, 2014
Position Description:
From Daily News December 23, 2013
Office of the Commercial Counsellor is looking to recruit a Secretary
Responsibilities
Handling internal and external telephone communication
Arranging appointments and making bookings
Writing documents and reports
Facilitates people who visits office
Performs such related duties given by Counsellor
Qualifications
At least diploma course
Applicants must be fluent in Kiswahili and English and be presentable and responsive.
Computer skills. (MS Windows and Office)
To have clear criminal record.
To be mentally and physically fit.
Application Instructions:
Qualified candidates who wish to apply for this role must submit a CV and cover letter to the Email Link above with the word “Secretary” as the subject. Deadline 8th January, 2014.
Do not send copies of certificates. Only shortlisted candidates will be contacted by office of Commercial Counsellors
NSSF YACHANGIA MILIONI 100 MFUKO WA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI ZANZIBAR
Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi la Zanzibar (SMZ), Dk. Mohamed Shein
akimkabidhi tuzo Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya
Jamii (NSSF), Chiku Matesa kutokana na kutambua mchango wa shirika hilo wa kuchangia sh. milioni
100 wakati wa uzinduzi wa Mfuko wa Uwezeshaji wa Wananchi Kiuchumi Zanzibar, uliokwenda sambamba na harambee ya kuchangia mfuko huo. Hafla
hiyo ilifanyika mjini Zanzibar, mwishoni mwa wiki.
Subscribe to:
Posts (Atom)